Psalms 63:3-8


3 aKwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai,
midomo yangu itakuadhimisha.

4 bNitakusifu siku zote za maisha yangu,
na kwa jina lako nitainua mikono yangu.

5 cNafsi yangu itatoshelezwa
kama kwa wingi wa vyakula;
kwa midomo iimbayo
kinywa changu kitakusifu wewe.


6 dKitandani mwangu ninakukumbuka wewe,
ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.

7 eKwa sababu wewe ndiwe msaada wangu,
chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.

8 fNafsi yangu inaambatana nawe,
mkono wako wa kuume hunishika.

Copyright information for SwhKC